Sunday , 30th Oct , 2022

Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amewahimiza wananchi kujitokeza katika uzinduzi wa matokeo ya mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi, utakaofanyika kesho Oktoba 31, 2022. Matokeo hayo ya sensa yatazinduliwa na Rais Samia.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule

Kauli hiyo ameitoa hii leo Oktoba 30, 2022 na kusema kuanzia majira ya saa 3:00 usiku wa leo kutakuwa na mkesha jijini humo.

"Leo kuanzia saa 3 hadi saa 6:00 usiku, tutakuwa na mkesha kuelekea uzinduzi wa matokeo ya mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022, pamoja na mwongozo wa  Kitaifa wa matumizi ya matokea ya Sensa, na mafataki yatakuwepo kuashiria utayari wa  wananchi Katika jambo hili muhimu," amesema RC Senyamule