
Jimbo hilo limekabiliana na uasi wa kikatili wa wanajihadi ambao umesababisha mzozo mkubwa wa kibinadamu kaskazini mwa Msumbiji.
Rais Filipe Nyusi mwezi Septemba alitangaza msamaha kwa wanajihadi wote waliojisalimisha wakati wa ziara yake katika jimbo hilo.
Tangu mwaka 2017, wanamgambo wamefanya ukatili mkubwa ikiwemo utekaji nyara, kukata watu vichwa, na kuchomwa kwa nyumba katika jimbo hilo na kuwalazimisha mamia kwa maelfu kukimbilia usalama wao.