Monday , 7th Nov , 2022

Wakili wa Upande wa utetezi katika kesi namba 2 inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya Wakili Helleni Mahuna  ameiambia Mahakama kuwa Sabaya ni mgonjwa na ana tatizo la moyo na kusisitiza kusikilizwa kwa kesi hiyo kwani imekaa muda mrefu

 Hakimu Erasto Phili amesema  kesi hiyo imedumu kwa muda mrefu na kuwataka upande wa Jamhuri kama cetifiketi zipo ni vyema zikawasilishwa mahakamani kwani  hakimu mwenye dhamana ya kusikiliza kesi hiyo ambaye ni hakimu Salome Mshasha yupo mafunzoni kwa takribani wiki moja  ili baada ya mafunzo hayo kesi hiyo ipate kusikilizwa
Hakimu phil ameihairisha kesi hiyo mpaka tarehe 21 mwezi wa 11  2022  na mshtakiwa ataendelea kuwa mahabusu