
Huu ni mwendelezo na timu imefika Tabata Jijini Dar es Salaam harakati zinaendelea kuvisaka na kuvirudisha katika ramani visima Ili kuepuka adha ya maji iliyopo Kwa sasa jijini Dar-Es-Salaam katika ufufuzi huo Afisa mwenezi kutoka DDCA Renatus Manoga amesecma kwamba zoezi hilo limeanza rasmi ijumaa ya wiki iliyopita na tayari vimeshaunganishwa kwenye mtandao wa DAWASA.
Wataalamu hao kutoka serikalini wamesema mashine wanazotumia kufufua visima hivyo zinauwezo wa kuchimba Hadi mita mia nne hamsini kwenda chini.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa kisiwani kata ya Tabata Alhaj Rajib mbwana Chala ameeleza kwamba kisima hicho kilikuwepo tangu miaka kumi na tano iliyopita na kilikuwa hakitumiki baada ya kupatikana Kwa maji ya dawasa hivyo kufufuliwa kwake kutatua changamoto ya uhaba wa Maji Kwa wakazi wa eneo hilo.