Sunday , 13th Nov , 2022

Watu sita wamefariki dunia hii leo Novemba 13, 2022, na wengine 22 kujeruhiwa jijini Dodoma kufuatia ajali iliyohusisha basi la Arusha Express na Lori la mchanga katika eneo la Mzakwe jijini humo.

Basi la abiria lililopata ajali

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kwamba kati ya sita waliofariki dunia, wanne wametambulika na waliojeruhiwa wanawake ni 10 na wanaume 12.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa mkoa wa Dodoma, Dkt Ernest, amesema kwamba majeruhi 17 waliopokelewa katika hospitali hiyo wanaendelea vizuri.