
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameyasema hayo alipokuwa akitoa salamu za Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye ufunguzi wa kongamano la uwekezaji katika sekta ya utalii mkoani Iringa.
Amesema Tanzania imejaliwa kuwa na vizutio vingi, Bara na Visiwani, hivyo wawekezaji wa ndani na nje wachangamkie fursa hiyo kwani baada ya Janga la UVIKO 19 nchi imefunguka na watalii wanaingia kwa wingi nchini ambapo wanahitaji huduma mbalimbali.
Aidha, katika kongamano hilo lililofunguliwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Mhe. Othman Masoud, Mhe. Balozi Dkt. Chana, amewaahidi wawekezaji kuwa, Wizara anayoiongoza itaendelea kushirikiana nao, katika kuweka Mazingira mazuri na rafiki ya uwekezaji katika Sekta ya Utalii nchini.