Monday , 14th Nov , 2022

Rais wa Marekani Joe Biden leo Novemba 14 amekutana na  Rais wa China Xi Jinping katika mji wa Bali, Indonesia kwa ajili ya kujadili mahusiano kati ya nchi hizo mbili 

Rais wa Marekani Joe Biden katika hotuba yake amezungumzia  umuhimu wa kuepuka migogoro kati ya Marekani na China huku akisema ni muhimu nchi hizo zifanye kazi pamoja katika masuala ya dharura ya kimataifa ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa na ukosefu wa usalama

Mkutano huu unafanyika pembezoni mwa mkutano wa nchi ishirini zilizoendelea na zinazoendelea kiviwanda G20 na ndio wa kwanza kwa viongozi hao wawili kukutana ana kwa ana tangu Biden alipochukua hatamu za uongozi Marekani.