Monday , 14th Nov , 2022

Siku moja baada ya vikosi vya Ukraine kuingia katika mji wa Kherson uliokuwa umechukuliwa na vikosi vya Urusi, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametembelea mji huo na kusisitiza kuwa vikosi vyake vinasonga mbele kukomboa miji iliyokuwa chini ya Urusi

Aidha Rais huyo amesema kuwa Ukraine ipo tayari kwa amani lakini iwe amani ya nchi yake yote

Jumamosi, umati wa watu ulisherehekea ukombozi wa mji wa Kherson baada ya vikosi vya Ukraine kuingia katika mji mkuu wa mkoa na wanajeshi wa Urusi kurudi mashariki.