Friday , 18th Nov , 2022

Mwanamke mmoja nchini Nigeria aliyemchukua mume wa rafiki yake na kuolewa yeye ameachwa na mwanaume huyo mara baada ya kujifungua.

Pete za ndoa

Kupitia ukurasa wa Twitter wa Ufuoma umeeleza kwamba mwanamke huyo huyo baada ya kuachwa kwa talaka mara baada ya kujifungua amezindua kitabu kinachoelezea masaibu aliyokutana nayo ndani ya ndoa na mwanaume huyo huku yeye akijiona mwanamke wa shoka.

"Huyu mwanamke aliolewa na mume wa rafiki yake na baadaye mwanaume huyo alimtelekeza baada tu ya kujifungua na kumpa talaka na sasa anazindua kitabu cha maisha yake kuonesha kwamba ni mwanamke shupavu," amesimulia Ufuoma.