
Silaha haramu zitakazoteketezwa
Taarifa hiyo imetolewa leo Novemba 20, 2022, na Msemaji wa Jeshi la Polisi SACP David Misime, ambapo amebainisha kuwa zoezi hilo litafanyika kuanzia muda wa saa 2:00 asubuhi katika viwanja vya shabaha vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) vilivyopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.
Aidha amebainisha kuwa Mgeni rasmi katika zoezi hilo anatarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Jumanne Sagini, na wananchi wote wanakaribishwa kujionea.