Friday , 16th Dec , 2022

Wizara ya mambo ya nje ya Urusi imeionya Marekani kuhusu mpango wake wa kuisaidia Ukraine  silaha za kisasa za kulinda anga lake

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Urusi Maria Zakharova

Urusi imesema kuwa kitendo cha Marekani kuisaidia Ukraine ni kama uchokozi na hawatasita kujibu 

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Urusi Maria Zakharova, amesema hatua ya Marekani kupeleka makombora ya kujilinda na kunasa makombora ya Urusi ni kama marekani inatangaza kuingia moja kwa moja katika mgogoro 

Tayari Marekani imetoa mafunzo kwa karibu wanajeshi 3,100 wa Ukraine, namna ya kutumia silaha hizo
Wakati hayo yakijiri tayari Marekani imewekea Russia vikwazo vipya vya kiuchumi na safari hii vimemlenga  mfanyabiashara tajiri nchini humo Vladimir Potanin na familia yake

Hatua hiyo inalenga kuishinkiza Moscow kuachana na vita vyake nchini Ukraine.

Potanin, aliwahi kuwa naibu wa waziri mkuu wa Russia, na Marekani imesema kwamba ana uhusiano wa moja kwa moja na rais wa Russia Vladimir Putin.

Wizara ya fedha ya Marekani pia imewekea vikwazo benki ya biashara ya Russia ya Rosbank ambayo Potanin alipata haki za umiliki wake mapema mwaka huu pamoja matawi 17 ya benki ya VTB ambayo ndio benki kubwa zaidi nchini Russia