Tuesday , 27th Dec , 2022

Jumla ya tani zipatazo 26  za korosho zilizobanguliwa, pamoja na tani moja ya nyama ya mabibo, zinatarajiwa kusafirishwa kwenda nchini Uholanzi na Ujerumani, baada ya kupatikana kwa soko la uhakika katika nchi hizo.

Korosho zilizobanguliwa

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Koroshi nchini, Francis Alfred, ambapo pamoja na mambo  mengine amesema, kupatikana kwa soko hilo kutaongeza thamani ya zao la korosho na kuongeza kipato kwa wakulima.

Awali mkuu wa wilaya ya Tandahimba Kanali Patrick Sawala, akawataka wakulima kuongeza uzalishaji, na kwamba kupitia uwekezaji huo, serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji, huku meneja wa kiwanda akaeleza kupitia ubanguaji huo, namna ambavyo  kiwanda hicho kimetoa ajira kwa wananchi.