Lengo kubwa ni pamoja na kusaidia kutunza mzingira na kuelimisha wanafunzi juu ya umuhimu wa mazingira.
Akizungumza wakati wa utekelezaji wa kampeni iliyopewa jina la panda mti ishi kijani, ambayo ilianza katika shule ya sekondari ya shushila ladwa iliyopo bagamoyo mkoani pwani, ambapo jumla ya miti 100 ilipandwa, Mkuu wa mkitengo cha masoko na mawasiliano kutoka VIVO ENERGY Bi. Grace Kijo amesema kwamba Mpango ni kuendeleza kampeni hiyo kwenye shule mbalimbaali nchini na kwamba miti zaidi ya 1,000 inatarajiwa kupanda
Nae Saidi Ling’wala- ambaye ni Mkuu wa kitengo cha mazingira kutoka VIVO ENERGY , pamoja na Marco Masaka Meneja vilainishi VIVO ENERGY, w amesema kwamba wakati huu ambapo mabadiliko ya tabia nchi yanaathiri kilimo kutokana na ukosefu wa mvua, kampuni hiyo imedhamiria kuendeleza ikiwezekana kufikia nchi nzima, lengo likiwa ni kupunguza tatizo hilo
Nao wakizingumza kutoka shuleni hapo ambapo miti hiyo 100 imepandwa Meshack Jacob ambaye ni Mkuu wa sekondari Shushila Ladwa pamoja na Zephania Mtebe Mwanafunzi Shushila Ladwa wamesema kwamba watakua msitari wa mbele katika kuitunza miti hiyo ili iweze kudumu muda mrefu,na kwamba kupitia miti hiyo mazingira ya shule yataendelea kuwa bora






