Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dereva bodaboda auawa Lindi

Tuesday , 28th Mar , 2023

Watu wawili ambao hawajajulikana hadi sasa wamemshambulia na kumsababishia kifo kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Zulkif Hemedi ambaye ni dereva bodaboda mkoani Lindi

Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoani Lindi  Pili Mande amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ambapo amesema vijana hao wawili walimhadaa dereva bodaboda huyo na mwishowe kumjeruhi kwa kitu chenye ncha kali na kumsababishia kifo

Taarifa za wananchi na viongozi katika kijiji cha Nangaru zinasema, Bodaboda huyo ambaye kwa asili ni mzaliwa wa Kijiji cha Nangaru, alifuatana na abiria hao wawili ambao alielekea nao upande wa mashambani, lakini baada ya mda mfupi alifanikiwa kuwapigia simu rafiki zake aliowasabahi kijiweni na kuwataarifu kuwa, abiria wake wamemgeuka na kumshambulia vibaya kiasi cha kupoteza fahamu.

Inasemekana kuwa, walipomshambulia na kumwacha chini, walifanikiwa kumpora simu kubwa na kumwacha marehemu na simu ndogo ambayo hawakufahamu kama aliificha mfukoni. 

Baada ya kupiga simu na kuomba msaada, wasafirishaji wenzake walitoa taarifa kijijini na kufanya msako mkubwa hadi kijiji jirani ambapo  walifanikiwa kuzuia barabara lakini jitihada za kuwakamata wahalifu hao iligonga ukuta, kwani walifahamu njama ya wanakijiji na kuamua kuitelekeza pikipiki vichakani na kukimbia.

Jeshi la Polisi Mkoani Lindi linaendelea kufanya msako mkubwa ili kuwabaini wahalifu hao huku polisi wakiwataka Madereva bodaboda wote kuwa na umoja lakini pia kusoma alama za hatari mapema ili waweze kujilinda na kutoa taarifa wanapohisi wapo mashakani

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA