
Baada ya kuibiwa yalisafirishwa kutoka katika mradi huo kwa nia ya kwenda kuyauzwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma ACP- Marco G. Chilya amesema kuwa mafuta hayo yalikamatwa, ambapo watuhumiwa walipelekwa mahakamani ambapo baada ya kesi hiyo kumalizika kwa mtuhumiwa kupata adhabu ya kifungo, mahakama iliamuru mafuta hayo yarudishwe kwenye uongozi wa unaosimamia mradi ili waweze kuyatumia katika ujenzi huo unaoendelea katika kijiji hicho cha Amanimakolo.
Pamoja na hilo Kamanda Chilya ameendelea kutoa onyo kali kwa wale wote wanaoendelea kujihusisha na uhalifu wa wa kuhujumu mradi huo waache mara moja kwani Jeshi la Polisi Mkoa Ruvuma litahakikisha linawasaka, kuwakamata pamoja na kuwafikisha mahakamani kama ilivyokuwa kwa wahalifu wengine.
Jeshi hilo limewahakikishia Raia hao wa kigeni kuwa linaendelea kufanya Misako, doria na Operesheni mbalimbali kuhakikisha maeneo yote ya Mkoa yanakuwa salama ikiwa pamoja na eneo lao la Ujenzi wa barabara.