Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ni maarufu ila hawapo ''Instagram'' wala ''X''

Friday , 23rd Feb , 2024

Hawa ni baadhi ya watu maarufu duniani ambao hawapo katika mitandao ya kijamii ikiwemo Instgram na X zamani (Twitter) licha ya umaarufu na nguvu kubwa ya ushawishi waliyonayo hasa katika sanaa. Wapo waliowahi kuingia na kutoka kwasababu zao binafsi, na wengine hawakurudi tena mtandaoni

Jay-Z; licha ya kuwa mmoja kati ya wasanii wa Hip Hop wenye ushawishi zaidi duniani huwezi kumpata Instagram wala X. Japo amewahi kujaribu kufungua akaunti Instagram na kuifuta baada ya saa chache tu, mfano Nov 2021 pia kuna akaunti iliyo Verified kwa jina la Mr.Carter kwenye X ambayo haimilikiwi na Jay Z.  Amezaliwa mwaka 1969.
-
Eddy Murphy; Mchekeshaji na mwigizaji maarufu duniani kutoka Marekani; hayupo katika mtandao wowote kuanzia Facebook, X wala Instagram. Amezaliwa mwaka 1961.
-
Jennifer Lawrence; Mwigizaji maarufu wa Marekani amabye hatumii mtandao wowote wa kijamii, hayupo Instagram wala X. Jennifer amezaliwa mwaka 1990.
-
Merghan Markle ambaye ni mke wa Mwanamfalme (Prince Harry) wa Uingereza, aliolewa mwaka 2018 na hapo kabla alikuwa Mwigizaji na Mhamasishaji, hana akaunti yoyote ya mtandao wa kijamii. Merghan amezaliwa mwaka 1981.
-
Tom Holland; Mwigizaji maarufu kutokea Uingereza, alitangaza kuchukua break ya kutokutumia mitandao ya kijamii tangu mwaka 2022 ili kukabiliana na changamoto ya afya ya akili iliyokuwa ikimkabili. Tom amezaliwa mwaka 1996.
-
Brad Pitt; Mwigizaji maarufu na Mtayarishaji mkongwe wa filamu nchini Marekani, hatumii mtandao wowote wa kijamii. Amezaliwa mwaka 1963.
-
Emma Stone; Mwigizaji maarufu wa kike na Mtayarishaji wa filamu nchini Marekani, hayupo katika mtandao wowote. Amezaliwa mwaka 1988.
-
Emily Blunt; licha ya mumewe John Krasinski kuwa katika mtandao wa Instagram, Emily Blunt ambaye ni mwigizaji maarufu kutokea Uingereza, yeye hatumii mtandao wowote wa kijamii na mara kadhaa amewahi kunukuliwa akisema anaishi kwa furaha. Emily amezaliwa mwaka 1983.
-
Tutajie mastaa wa hapa Bongo unaowafahamu hawapo katika mitandao yoyote ya kijamii.

HABARI ZAIDI

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato