
Shai Gilgeous-Alexander
Ameshinda tuzo hii baada ya kuisaidia timu yake ya The Oklahoma City Thunder kushinda ubingwa wa NBA msimu huu 2024-25 baada ya kushinda mchezo wa saba wa fainali leo alfajiri kwa kuifunga Indiana Paceres kwa alama 103-91, na kushinda fainali kwa ushindi wa michezo 4-3.
Kwenye mchezo huu wa saba Shai Gilgeous-Alexander amecheza dakika 40, kafunga alama 29, katoa pasi za kufunga (assist) 12 na mipira iliyorudi yani reboundi 5.