Mbunge wa Kenya atekwa, akutwa kwenye shamba
Mbunge wa Juja nchini Kenya George Koimburi, amekutwa ametupwa akiwa hai katikati ya shamba la kahawa katika kaunti ya Kiambu nchini humo, baada ya jana Jumapili Mei 25, 2025, kukamatwa na watu wasiojulikana nje ya kanisa katika eneo la Mugutha.