Murray arejea 100 bora kwenye Tennis
Nyota wa tennis kutoka England, Andy Murray amerejea kwenye 100 bora ya viwango vya tennis Duniani kwa wanaume baada ya kukosekana tangu mwaka 2018 alipopata ushindi dhidi ya Mkazakhstan Alexander Bublik kwa seti 2-0 katika michuano ya Rotterdam nchini Uholanzi .
