Viongozi wanyanyua mabega waonywa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali kujikweza na kunyanyua mabega kiutawala na kuacha kuwasaidia wananchi ambao ndo waajiri wao katika huduma mbalimbali.

