DC Kisarawe, Nikk wa Pili aanza na wajawazito
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mhe. Nickson Simon ameendesha zoezi la uchangishaji damu katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe, ikiwa ni sehemu ya kutatua changamoto kubwa ya vifo vinavyotokana na upungufu wa damu inayowakabili akina mama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.

