Rais aagiza Walimu 6000 waajiriwe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu amewataka Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) kujaza nafasi za walimu zaidi ya 6000 wanaohitajika kutokana na walimu hao wengine kustaafu na wengine kufariki na nafasi zao hazijazibwa tena.