Fundi afa kwa shoti akichomelea
Mkazi wa Mtaa wa Kazaroho, Kata ya Mbugani katika Manispaa ya Tabora, Salumu Madinda amepoteza maisha papo hapo baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakati akichomelea sehemu iliyopasuka kwenye bodi la gari kwa kutumia mtambo wa kuchomelea (welding machine).