"Nisamehe huko ulipo" - Msanii TID
Ikiwa leo ni siku ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, msanii wa BongoFleva TID amemuomba msamaha Hayati Magufuli kwa kushindwa kufika kwenye msiba wake Wilayani Chato Mkoani Geita.