Mzee wa miaka 77 afariki kisimani
Mzee mmoja aliyefahamika kwa majina ya Joseph Rutabana mwenye umri wa miaka 77 mkazi wa kijiji cha Butairuka amepoteza maisha, baada ya kutumbukia katika kisima cha maji, kilichochimbwa katika eneo la Kanisa Katoliki Parokia ya Maruku, katika halmashauri ya wilaya ya Bukoba, mkoani Kagera.