Mgombea Urais, Demokrasia Makini kukomesha ubakaji
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia Makini Mh. Cecilia Mmanga amesema endapo atapata ridhaa ya kuliongoza taifa la Tanzania atahakikisha watuhumiwa wa makosa ya ubakaji na ulawiti wanapewa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.