Mvua Dar, mbogamboga zimesombwa na maji
Baada ya mvua kubwa kunyesha jana Jijini Dar es Salaam, imepelekea mboga za majani kuadimika sokoni leo hali iliyopelekea fungu moja la matembele kuuzwa kati ya mia tisa hadi elfu moja na mia mbili, huku mchicha na maboga ukiuzwa shilingi 500.