'Polisi haina pesa ya kufunga CCTV' - Masauni
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, amewataka Wabunge kushirikiana na wadau mbalimbali katika maeneo yao kwa lengo la kuhakikisha wanachangia upatikanaji wa CCTV Camera, zitakazofungwa katika vituo vya polisi nchini ili kuepusha malalamiko ya wananchi.