Maadhimisho mengine ya kitaifa yafutwa
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni amesema Baraza la Taifa la Usalama Barabarani limeifuta wiki ya nenda kwa usalama barabarani iliyokuwa ikifanyika kila mwaka kwa madai imekuwa ikitumia gharama kubwa huku ajali zikiendelea kuwepo.