Simba SC yamwandikia barua Waziri Jafo
Kuelekea mchezo wa klabu bingwa Afrika kati ya Simba SC dhidi ya Mbabane Swallows utakaopigwa Jumatano, Novemba 28 jijini Dar es salaam, klabu ya Simba imemuomba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo, awe mgeni rasmi.