Kangi Lugola aibukia Zanzibar
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameibuka visiwani Zanzibar kwa ajili ya ziara ya Kikazi visiwani humo ambapo amekutana na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais wa Zanzibar Dkt Ally Mohamed Shein.