CAG abaini matumizi mabaya ya misamaha ya kodi
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Prof. Mussa Assad, imebaini kuwapo kwa matumizi mabaya ya msamaha wa kodi wa shilingi bilioni 3.46, uliotolewa kwa walengwa wawili walioagiza jumla ya magari 238 mwaka wa fedha wa 2015/16.