TFF yasubiri hukumu ya CAF kuhusu kijeba wa Congo
Shirikisho la soka nchini Tanzania, TFF, limewataka watanzania kutulia na kusubiri maamuzi ya Shirikisho la soka Afrika CAF, juu ya kushindwa kwa Congo kupeleka mchezaji wao Langa Lesse Bercy, kwenye vipimo jijini Cairo.

