Serikali yatoa neno Mtanzania aliyefia Urusi
Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Stergomena Tax, amesema Mtanzania aliyefariki dunia nchini Urusi Nemes Tarimo, alikuwepo nchini humo kwa ajili ya masomo na alijiunga na chuo cha Moscow Technology Pro mwaka 2020 kwa masomo ya shahada ya uzamili katika fani ya Business Informatics.

