Aziz Ki atemwa kikosi cha Burkina Faso

Kikosi cha Yanga SC kina Wachezaji wengi wanaoweza kuziba pengo la Aziz Ki kipindi atakachokosekana uwanjani ili atafute utimamu wa mwili wake Clatous Chama na Pacôme Zouzoua ni mbadala sahihi kwenye eneo la namba 10 kikosi cha Wanachi.

Kocha wa timu ya taifa ya Burkina Faso Brama Traoré ametaja majina ya Wachezaji atakawatumia kwenye michezo miwili ya kufuzu AFCON 2025, dhidi ya timu za taifa za Senegal na Malawi jina la Mchezaji wa Yanga ya Tanzania Stephane Aziz Ki likikosekana kwenye kikosi hiko.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS