Afisa Uendeshaji wa Taasisi ya Under The Same Sun Gamariel Mboya (kulia) akiwa na Mkurugenzi wa taasisi hiyo Bi. Vicky Ntetema.
Watanzania wametakiwa kuungana kuwafichua watu wanojihusisha na vitendo vya ukatili ikiwemo kuwakata viungo na kuwauwa watu wenye ulemavu wa ngozi maarufu kama albino.