Amchana Mwanaye kwa Wembe aweze kujisaidia
Mkazi wa Kata ya Kitangiri katika Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza, Anastazia Ngilitu, amemchana kwa wembe mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili na wiki mbili baada ya mtoto huyo kuzaliwa bila kuwa na sehemu ya haja kubwa
Aidha, amebainisha kuwa wakati wa kujifungua, mtoto huyo alifanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Bugando na kuwa baada ya muda mchache hali hiyo ilijirudia na kuamua kumnasua kwa kumchana bila kujua madhara ya aina yeyote ambayo yangeweza kumpata mtoto wake ambapo kwa sasa afya ya mtoto hairidhishi baada ya kuchanwa.