Daddy Owen aonesha usamaria.
Mwanamuziki wa Kenya, Daddy Owen ameendelea kuonesha moyo wake wa ukarimu kupitia taasisi yake ya hisani ya Malaika Trust, ambapo safari hii ameamua kujitolea kulipa gharama za masomo za binti mwenye tatizo la macho, ambaye anaitwa Dais Kangogo.