Daniel Dubois kutetea mkanda wake dhidi ya Wardley

Bingwa wa masumbwi kwa uzito wa juu ( heavyweight ) anayeshikilia mkanda wa Shirikisho la kimataifa la  ngumi Duniani IBF, Daniel Dubois amepewa muda wa kuamua Mpinzani atakayekutana naye kwenye pambano la kutetea ubingwa wake alioupata mwezi Septemba  baada ya kumshinda  Anthony Joshua.

 Fabio Wardley anatizamwa kama Bondia sahihi wa kupanda ulingoni dhidi ya Dubois kutokana na uwezo wake mkubwa ulingoni na rekodi zake. Ameshinda mapambano 17 kwa KO kati ya 18 aliyopigana huku Daniel Dubois akiwa na rekodi ya   KO 21 kati ya mapambano 22 aliyopiyogana.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS