Kenzo; Sasa mambo shwari
Msanii Kenzo wa nchini Kenya ameweka wazi kuwa baada ya kipindi cha changamoto kubwa kwa fani yake ya muziki, ambapo alipoteza mkataba na lebo ya Ogopa, kwa sasa anaona mwanga katika muziki wake akiwa msanii huru anayeweza kufanya kazi mahali popote.