Simbachawene akerwa na wanaofokea watumishi wenzao
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene ameonesha kukerwa na baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi za Serikali wenye tabia ya kuwafokea Watumishi walio chini yao wakiamini kufanya hivyo ndio uongozi.