Juma Mwambusi atangazwa Kocha Mkuu Coastal Union

Klabu ya Coastal Union ya Tanga imemtangaza Juma Mwambusi kuwa kocha mkuu wa timu hiyo baada ya kumfuta kazi aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo David Ouma raia wa Kenya mwezi Agosti 2024. Kikosi hiko cha Wagosi wa Kaya kilikuwa chini ya Joseph Lazarao ambaye alikaimu kwa muda kipindi ambacho timu hiyo ilipokuwa inatafuta Mwalimu Mkuu.
Mwambusi anauzoefu mkubwa wa kufundisha ligi Kuu ya Tanzania baada ya kuhudumu kwenye nafasi ya Kocha mkuu na Msaidizi kwenye timu mbalimbali nchini. Kocha Mwambusi amewahi kufundisha Mbeya City, Yanga, Azam pamoja na Ihefu.