Wachezaji waijia juu FIFA udhamini wa Waarabu

Wachezaji wa timu za taifa za Wanawake zaidi ya 100 wameliandikia barua ya wazi Shirikisho la mpira Duniani FIFA kulitaka kuvunja mkataba wake wa udhamini na kampuni ya mafuta ya Saudi Arabia ya Aramco. Sababu kubwa zilizotajwa na Wachezaji hao ni kutokana na uharibifu wa Mazingira unaofanywa na kampuni hiyo ya uchimbaji wa mafuta, pamoja na uvunjwaji wa Haki za Binadamu nchini SaudI Arabia. Uwepo wa tamaduni ambazo zinamkandamiza Mwanamke nchini humo inatizamwa kama sababu kubwa zaidi ya Wachezaji wa timu za Wanawake kugomea mkataba huo wa udhamini. Aramco imesaini mkataba na FIFA utakaofika tamati mwaka 2027 ambapo kampuni hiyo itadhamini kombe la Dunia la Wanaume 2026 na Wanawake 2027.

Wachezaji wa timu za taifa za Wanawake wamepiga kura kulishinikiza Shirikisho la mpira Duniani FIFA kuvunja ushirikiano wa kiudhanini na kampuni ya mafuta ya Saudi Arabia Aramco. Saudi Arabia inatuhumiwa kwa uvunjifu wa Haki za Binadamu na kuwepo kwa tamaduni kandamizi kwa Wanawake.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS