Ramadhani Kayoko Hakimu Simba SC VS Yanga SC

Bodi ya ligi kuu Tanzania bara imemtangaza Ramadhani Kayoko kusimamia sheria kumi na saba kwenye mchezo wa Dabi ya Kariakoo mchezo unaozikutanisha timu za Simba SC dhidi ya Yanga SC katika uwanja wa Benjamini Mkapa. Mchezo huo mkubwa nchini Tanzania na Afrika ya Masharaiki utachezwa kesho Jumamosi saa 11:00 jioni. Watakaomsaidia Kayoko ni Mohamed Mkono kutoka Tanga na Kassim Mpanga huku Tatu Malogo atakuWa Muamuzi wa mezani.
Ramadhani Kayoko amepewa jukumu la kusimamia mchezo wa Simba SC dhidi ya Yanga SC siku ya kesho saa 11:00 jioni uwanja wa Benjamini Mkapa Jijini Dar es salaam. Simba SC itakuwa wenyeji wa mchezo huo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu Tanzania bara.