Maafisa ugani watakiwa kufika vijijini.
Baadhi ya wakulima wa mazao mbalimbali katika Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, wameiomba serikali kuongeza idadi ya maafisa ugani vijijini, ili waweze kuwatembelea kwa wakati kuwahamasisha kulima mazao mengine ya biashara, na kuwapatia elimu juu ya matumizi bora ya mbolea.