Nyumba yateketea Dodoma, chanzo chatajwa
Moto umeteketeza nyumba yenye vyumba sita hii leo Septemba Mosi, 2022, eneo la Kata ya Chamwino Chinangali Jijini Dodoma, na kuunguza vitu vyote vilivyomo ndani ya nyumba hiyo, huku chanzo kikitajwa kuwa ni kuvuja kwa gesi ambayo hewa yake ilikutana na joto la mkaa.