Omanyala ashinda dhahabu Jumuiya ya Madola
Mwanariadha wa Kenya wa mbio fupi za mita mia moja Ferdinand Omanyala ameushangaza ulimwengu baada ya kuibuka mshindi na kutwaa medali ya dhahabu katika michezo ya nchi za Jumuiya ya Madola inayoendelea mjini Birmingham nchini Uingereza.