Vijana washauriwa kupima afya zao
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Sahili Nyanzabara Geraruma, amewataka Watanzania hasa vijana wa kike na kiume kupima afya zao, vikiwamo virusi vinavyosababisha maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi (VVU), kwani vijana wengi wanaangamia na ugonjwa huo hatari.