Tembo wavamia makazi ya watu Lindi
Tembo wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 50 wameweka kambi katika kata ya Mkoka wilayani Nachingwea Mkoani Lindi, wakionekana kutafuta chakula wakitokea porini, jambo lililowafanya wanakijiji wa kata hiyo kukaa macho kwa takribani saa 08 kwa kuhofia usalama wao na mali zao.