Mnamo Januari 2020, Jennie Barber alikata tiketi mbili za ndege za kurudi Japan zikiondoka mwezi Mei , lakini baadaye ndege hizo ziliondolewa kutokana na vizuizi vya Covid. Shirika hilo la dnege ilitoa marejesho kwa njia ya vocha za usafiri lakini Bi Barber alitaka pesa zake zirejeshwe na Shirika la ndege lilikataa.
Akijiwakilisha mwenyewe, Bi Barber alilipeleka shirika hilo mahakamani na kushinda marejesho yake kamili. Mwanamama huyo emenukuliwa akisema kwamba "Kama upo. mtu wa kawaida, ambaye si mtaalamu wa sheria, kwenda mahakamani kupambana na mtu kama British Airways inatisha ‘’
Hata hivyo, Bi Barber, ambaye alisomea sheria ya kiwango cha A, aliweza kuishinda kampuni hiyo kubwa ya ndege mahakamani kwa kutumia Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya mwaka 1943.




.jpg?itok=5cvL0YaP)

